Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashirika ya afya yanaomba kufadhiliwa misaada ziada kupambana na homa ya manjano

Mashirika ya afya yanaomba kufadhiliwa misaada ziada kupambana na homa ya manjano

Mashirika ya UM juu ya maendeleo ya watoto, UNICEF, na afya, WHO, yameonya kwamba akiba ya dharura ya chanjo dhidi ya homa ya manjano katika Afrika imo hatarini ya kumalizika mwaka ujao, kwa sababu ya upungufu wa misaada ya kufadhilia uzalishaji wa dawa hizo kutoka wahisani wa kimataifa.