Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

IGAD inaliomba BU kuweka vikwazo dhidi ya anga ya Usomali

IGAD inaliomba BU kuweka vikwazo dhidi ya anga ya Usomali

Taasisi juu ya Maendeleo baina ya Serikali za Afrika Mashariki, (IGAD) imelitumia Baraza la Usalama (BU) ombi la kuitaka ipige marufuku ndege zote kuruka kwenye anga ya Usomali, kwa makusudio ya kuwanyima wale waliotambuliwa kama "wadhamini na wafadhili wa kigeni" fursa ya kupeleka silaha, marisasi na baruti nchini humo.