20 Mei 2009
Dktr Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) ameripoti ya kuwa hali ya kawaida ikijiri, kuna uwezekano kwa makampuni ya madawa ya kimataifa yakamudu kuharakisha utengenezaji wa dozi bilioni 4.9 za chanjo dhidi ya vimelea vya homa mpya ya mafua ya H1N1 katika kipindi cha mwaka mmoja.