Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mashitaka mapya dhidi ya Aung San Suu Kyi yalaumiwa na Navi Pillay

Mashitaka mapya dhidi ya Aung San Suu Kyi yalaumiwa na Navi Pillay

Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu, Navi Pillay, Ijumaa alishtumu taarifa zilizoonyesha kwamba wenye mamlaka Myanmar walimfungulia mashitaka mapya mpinzani, Aung San Suu Kyi. Aliwasihi kufuta msururu wa mashitaka ambayo yanafungamana na tukio nje ya uwezo wa Aung San Suu Kyi.

Pillay aliwasihi wenye madaraka Myanmar kumwachia, haraka, Aung San Suu Kyi kutoka uzuizi unaoendelea, kitendo ambacho, alisisitiza, hutengua sheria za kitaifa za Myanmar, yenyewe, halkadhalika, na pia huvunja misingi ya "sheria ya kimataifa ya usikilizaji wa mashitaka na haki ya kujitetetea" ya mtuhumiwa.