BU, Umoja wa Afrika waafikiana kuimarisha ushirikiano
Mwisho wa wiki iliopita, mnamo Ijumamosi ya tarehe 16 Mei (2009), wajumbe wa Baraza la Usalama wa kutoka Makao Makuu ya UM, walipokuwepo Addis Ababa, Ethiopia kwenye ziara yao ya Afrika, walikuwa na mazungumzo na wawakilishi wa Baraza la Usalama na Amani la Umoja wa Afrika ambapo waliafikiana kushauriana, kwa ukaribu zaidi, na kushirikiana kwenye juhudi za kuzuia na kusuluhisha mizozo iliyotawanyika Afrika kwa sasa, na vile vile walikubaliana kujumuisha mchango wao katika huduma za kulinda amani na kudumisha utulivu kwenye maeneo yote husika.