Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mfuko wa maafa ya dharura waipatia Kenya dola milioni 8.6 kuhudumia misaada ya kihali

Mfuko wa maafa ya dharura waipatia Kenya dola milioni 8.6 kuhudumia misaada ya kihali

John Holmes, Mratibu Mkuu wa UM juu ya Misaada ya Dharura, ameidhinisha dola milioni 8.6 zitolewe kutoka Mfuko wa UM wa Maafa ya Dharura au Mfuko wa CERF, ili kufadhilia miradi ya kuwavua mamia elfu ya watu nchini Kenya na matatizo ya ukame, bei ya juu ya chakula duniani, na kujistiri kimaisha na mabaki ya athari za vurugu la baada ya uchaguzi, pamoja na kudhibiti mripuko wa maradhi ya kipindupindu, na vile vile kukidhi mahitaji ya umma wa Usomali uliopo Kenya kwa sababu ya mifumko ya mapigano nchini mwao.