Riporti ya WHO kuhusu maambukizi ya homa ya H1N1
Takwimu mpya za maambukizo ya homa ya mafua ya A(H1N1) ulimwenguni, zilizothibitishwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) mnamo Ijumaa ya tarehe 08 Mei (2009) ni kama ifuatavyo: Jumla ya watu 2500 waliripotiwa rasmi kuambukizwa na homa ya mafua ya H1N1 katika mataifa 25, ikijumlisha Brazil, kwa mara ya kwanza tangu tatizo hili la afya kuzuka.