Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO/UNEP yahadharisha dhidi ya athari haribifu kutoka 'uvuvi wa mapepo' baharini

FAO/UNEP yahadharisha dhidi ya athari haribifu kutoka 'uvuvi wa mapepo' baharini

Taarifa mpya, iliotolewa kwa pamoja baina ya Shirika a UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) na Shirika la Hifadhi ya Mazingira (UNEP) imehadharisha juu ya kuselelea kwa hatari ya kimazingira na biashara, inayochochewa na vifaa vya uvuvi vilivyopotea au kutupwa baharini kihorera na wavuvi, vitu ambavyo vimethibitika huharibu sana maumbile ya baharini, na kuathiri bidhaa ya samaki kwa sababu ya uvuvi unaojulikana kama "uvuvi wa kizimwi na mapepo".