Orodha ya wagombea wadhifa wa Mkurugenzi Mkuu yatangazwa rasmi na IAEA
Shirika la UM Kuhudumia Matrumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) limetangaza kuwa limepokea orodha rasmi ya wagombea uchaguzi wa cheo cha Mkurugenzi Mkuu mpya wa taasisi hii ya kimataifa baada ya kiongozi wa sasa Mohamed ElBaradei kutangaza atastaafu atakapomaliza muda wake mwaka huu.