Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Nchi saba zimegundua waathirika wa homa ya mafua ya nguruwe, WHO imethibitisha

Nchi saba zimegundua waathirika wa homa ya mafua ya nguruwe, WHO imethibitisha

Mkurugenzi wa Taasisi ya Marekani ya Kudhibiti Maradhi (CDC) amenakiliwa na vyombo vya habari akithibitisha ripoti inayosema mtoto mchanga wa miezi 23, katika jimbo la Texas, amesajiliwa kufariki kufuatia maambukizo ya homa ya mafua ya nguruwe. Kifo hiki ni cha kwanza kutukia Marekani, miongoni mwa wale watu waliopatwa na ugonjwa huo.