Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano juu ya Mwito wa Durban Kupinga Ubaguzi wahitimishwa Geneva

Mkutano juu ya Mwito wa Durban Kupinga Ubaguzi wahitimishwa Geneva

Mkutano wa Mapitio juu ya Mwito wa Durban dhidi ya Ubaguzi, uliofanyika wiki hii mjini Geneva, Uswiss ulikamilisha shughuli zake leo Ijumaa. Kwenye mahojiano na waandishi habari wa kimataifa juu ya kikao hicho, Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Bindamau, Navi Pillay alisema anaamini Mkutano ulikuwa wa mafanikio makubwa, licha ya kwamba mapatano yalikuwa magumu na yalichukua muda mrefu kukamilishwa.