Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa Brussels juu ya Usomali waahidi mamilioni kufufua amani

Mkutano wa Brussels juu ya Usomali waahidi mamilioni kufufua amani

Kwenye Mkutano wa Kimataifa juu ya Usomali, uliofanyika kwenye mji wa Brussels, Ubelgiji Alkhamisi ya leo, wenye kuongozwa bia na Mwenyekiti wa UA, Jean Ping na KM wa UM Ban Ki-moon, uliwahamasisha wafadhili wa kimataifa kuahidi kuchangisha karibu dola milioni 250 kulisaidia taifa husika la Pembe ya Afrika kurudisha utulivu na amani ya eneo.