Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Abiria 35 wa mashua za magendo wameripotiwa na UNHCR kuzama Yemen

Abiria 35 wa mashua za magendo wameripotiwa na UNHCR kuzama Yemen

Taarifa ya Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) imeeleza kwamba watu 35 waliripotiwa kuzama Ijumatano kwenye mwambao wa jimbo la Abyan, Yemen, liliopo kilomita 250 mashariki ya Aden, baada ya moja ya mashua mbili za wafanya magendo kupinduka.