Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maambukizo ya Kipindupindu kusini mwa Afrika yaripotiwa kupungua na OCHA

Maambukizo ya Kipindupindu kusini mwa Afrika yaripotiwa kupungua na OCHA

Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti kuwepo mwelekeo wa kutia moyo kuhusu udhibiti wa maradhi ya kipindupindu kusini mwa Afrika. Ripoti imeeleza ya kuwa kasi ya maambukizo ya maradhi haya kieneo yanaendelea kuteremka.