Maambukizo ya Kipindupindu kusini mwa Afrika yaripotiwa kupungua na OCHA
Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) imeripoti kuwepo mwelekeo wa kutia moyo kuhusu udhibiti wa maradhi ya kipindupindu kusini mwa Afrika. Ripoti imeeleza ya kuwa kasi ya maambukizo ya maradhi haya kieneo yanaendelea kuteremka.