Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkuu wa UNHCR ashtumu sera za ubaguzi dhidi ya waombao hifadhi ya kisiasa

Mkuu wa UNHCR ashtumu sera za ubaguzi dhidi ya waombao hifadhi ya kisiasa

Ijumatano, Antonio Guterres, Kamishna Mkuu wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) aliwaambia wajumbe waliohudhuria Mkutano wa Geneva wa Mapitio ya Utekelezaji wa Mwito wa Durban Kupinga Ubaguzi Duniani, tangu kumalizika kwa Mkutano wa Awali wa Durban dhidi ya Ubaguzi miaka saba na nusu iliopita, waathirika wa mateso ulimwenguni bado wanaendelea kunyimwa hifadhi kwenye yale maeneo yenye uwezo wa kuupatia umma huo hali ya usalama.