Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Utatuzi Mbadala wa Mzozo wa Chakula Duniani

Utatuzi Mbadala wa Mzozo wa Chakula Duniani

Mnamo wiki hii, David Nabarro, aliyeteuliwa kuongoza Tume ya UM juu ya Mzozo wa Chakula Duniani amehadharisha kwamba licha ya kuwa,katika siku za karibuni bei za chakula duniani ziliteremka kwa kiwango kikubwa sana, tukio hilo halikufanikiwa kuuvua umma wa nchi masikini na tatizo la njaa. Mamilioni ya watu duniani bado hawana uwezo wa kupata chakula kwa sababu ya mchanganyiko wa ufukara na mporomoko, usio wa kawaida, wa shughuli za uchumi, kijumla.

Sikiliza ripoti kamili kwenye idhaa ya mtandao.