Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

KM asikitishwa na urushaji wa kombora angani na Korea Kaskazini

KM asikitishwa na urushaji wa kombora angani na Korea Kaskazini

Ofisi ya Msemaji wa KM, kwenye ripoti iliotoa Ijumapili kwa waandishi habari, kuhusu kitendo cha kurusha kombora angani kilichofanywa na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Umma wa Korea (Korea Kaskazini) hapo jana, taarifa hiyo ilibainisha masikitiko aliyokuwa nayo KM Ban Ki-moon juu ya kitendo cha Korea Kaskazini, ambacho alisema ilikwenda kinyume kabisa na nasaha za jumuiya ya kimataifa.