Vijana wa mjini kupata msaada kutoka mpango mpya wa UM
Kutokana na hali kwamba karibu robo tatu ya wakazi bilioni moja wa dunia wanaoishi kwenye vitongoji vya ufukara ni vijana chini ya miaka 30, shirika la Makazi la Umoja wa Mataifa limeanzisha mradi mpya wa kuwezesha makundi ya kijami yanayongozwa na vijana.