Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Pendekezo la FAO la Mkutano wa Viongozi juu ya Mzozo wa Chakula lapata Nguvu

Pendekezo la FAO la Mkutano wa Viongozi juu ya Mzozo wa Chakula lapata Nguvu

Shirika la Chakula na Kilimo Duniani FAO, limesema kwamba pendekezo la kuitisha mkutano wa viongozi duniani mwishoni mwaka 2009 juu ya mzozo wa chakula, ambao unazidi kuzorota katika nchi maskini, linapata nguvu na kupewa umuhimu mkubwa.