Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Majeshi ya UM yachukua udhibiti huko Chad kutoka kwa kikosi cha EU

Majeshi ya UM yachukua udhibiti huko Chad kutoka kwa kikosi cha EU

Walinda amani wa UM huko Chad na Jamhuri ya Afrika ya Kati walichukua udhibiti wa kijeshi na usalama kutoka kwa kikosi cha Ulaya katika mataifa mawili hayo yenye kukumbwa na ghasia.

Sherehe za kukabidhi mamlaka ya maeneo hayo yalifanyika katika mji wa mashariki mwa Chad wa Abeche na kuhudhuriwa na naibu katibu mkuu wa shughuli za kulinda amani Alain Le Roy. Mwezi Januari Baraza la Usalama liliidhinisha kupelekwa zaidi ya wanajeshi elfu 5 500 wakulinda amani, polisi 300, wanafanyakazi wa kijeshi 5 200, kutumikia ofisi ya UM huko kuchukua nafasi ya wanajeshi wa Ulaya walopelekwa huko tangu mwezi Marchi mwaka jana. Taarifa ya KM iliyotolewa na msemaji wake inapongeza kazi za wanajeshi wa Ulaya kuwalinda watu walopoteza makazi yao, wakimbizi na wakazi huko mashariki ya Chad na kaskazini mashariki ya Jamhuri ya Afrika ya Kati.