Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Libya itazingatia sera ya kulinda amani na Sudan wakati inaongoza Baraza la Usalama

Libya itazingatia sera ya kulinda amani na Sudan wakati inaongoza Baraza la Usalama

Libya inasema miongoni mwa masuala itazingatia mnamo mwezi huo inaposhikilia uwenyekiti wa Baraza la Usalama la UM ni sera ya kazi za kulinda amani na athari zinazoweza kutokea, kutokana na uwamuzi wa Mahakama ya Uhalifu ya Kimataifa kutoa kibali cha kukamatwa kwa Rais wa Sudan.

Balozi wa Libya Ibrahim Dabbashi, akizungumza kabla ya uwamuzi kutolewa amesema hakuna kikao maalum kilichopangwa kulijadili suala hilo hata hivyo amesema mashauriano kati ya wanachama wa baraza yanaendelea juu ya uwezekano wa kutumia kifungu cha 16 cha mkataba wa Rome uloanzisha ICC, kitakacho chelewesha uchunguzi kuhusiana na mashataka hayo kwa miezi 12. Alisema ni muhimu Baraza la Usalama litafakari suala hilo kuambatana na maamuzi yatakayochukuliwa na mashirika ya kikanda hasa Umoja wa Afrika na Umoja wa Nchi za Kiarabu.