Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

ICTR imethibitisha tena kifungo cha maisha kwa mtuhumiwa Karera

ICTR imethibitisha tena kifungo cha maisha kwa mtuhumiwa Karera

Mahakama ya Rufaa ya Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) imethibitisha tena kifungo cha maisha kwa mtuhumiwa François Karera, ambaye mnamo 07 Disemba 2007 alipatikana na hatia ya kushiriki kwenye mauaji ya halaiki, pamoja na maangamizi dhidi ya raia wenye jadi ya Kitutsi katika sekta ya Nyamirambo, wilaya ya Kigali Ville, na mauaji katika Kanisa la Ntarama mnamo 15 Aprili 1994, na pia kushiriki kwenye jinai dhidi ya utu iliofanyika katika kijiji cha Rushahi, kwenye Wilaya ya Kigali.