Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM umeanzisha kampeni ya kufufua huduma za kiuchumi na jamii Ghaza

UM umeanzisha kampeni ya kufufua huduma za kiuchumi na jamii Ghaza

Ijumatatu, mjini Geneva, John Holmes, Naibu KM juu ya Masuala ya Kiutu alianzisha rasmi kampeni ya kuchangisha msaada wa dola milioni 613, kutoka wahisani wa kimataifa, msaada unaohitajika kukidhi mahitaji ya kihali kwa waathirika wa mashambulizi ya karibuni ya vikosi vya Israel, yaliofanyika kwenye eneo liliokaliwa la WaFalastina la Tarafa ya Ghaza.