Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mwendesha mashitaka wa kesi ya Taylor ametangaza kukamilisha ushahidi

Mwendesha mashitaka wa kesi ya Taylor ametangaza kukamilisha ushahidi

Stephen Rapp, Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama Maalumu juu ya Jinai ya Vita katika Sierra Leone kwenye mahojiano ya Ijumatatu, na waandishi habari, hapa Makao Makuu alisema ya kwamba upande wa mashitaka umemaliza kuwasilisha ushahidi wa kesi dhidi ya Charles Taylor, aliyekuwa Raisi wa taifa jirani la Liberia.