KM ahimiza mataifa kujumuika kudhibiti kidharura mabadiliko ya hali ya hewa
KM Ban Ki-moon anahudhuria Mkutano Mkuu juu ya Maendeleo ya Kusarifika, unaofanyika mjini New Delhi, Bara Hindi ambapo aliwaambia wajumbe wa kimataifa waliokusanyika huko ya kuwa walimwengu wanawajibika kukabili, kipamoja, tishio hatari, linaloendelea kupanuka kimataifa, linalochochewa na athari za mabadiliko ya hali ya hewa duniani.