KM ahimiza uvumilivu baada ya maandamano Bukini kuzusha vifo
Ijumapili KM Ban Ki-moon, kwa kupitia msemaji wake, ametoa taarifa iliosihi makundi yanayohasimiana Bukini, kujitahidi kusuluhisha tofauti zao kwa amani. Alishtumu vikali fujo na vurugu lilioripuka Ijumamosi katika mji mkuu wa Antananarivo, ambapo inakisiwa watu 28 waliuawa na darzeni kadha walijeruhiwa.