Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUC yakataa hadharani madai ya Nkunda

MONUC yakataa hadharani madai ya Nkunda

Shirika la UM juu ya Ulinzi Amani katika JKK (MONUC) limeripoti kukanya madai ya Laurent Nkunda, kiongozi wa kundi la waasi wa CNDP aliyoyabainisha kwenye barua aliomtumia Mjumbe Maalumu wa KM, Alan Doss, madai yaliyosema kwamba vikosi vya Serikali vimeonekana kuongezwa kwenye ile sehemu ya mapigano, katika eneo la mashariki la Kibati, liliopo kilomita 10 kaskazini ya mji wa Goma.