Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNRWA yaomba dola milioni 34 kuhudumia misaada ya kiutu katika Ghaza

UNRWA yaomba dola milioni 34 kuhudumia misaada ya kiutu katika Ghaza

Shirika la UM Linalofarajia Wahamiaji wa KiFalastina katika Mashariki ya Karibu (UNRWA) limetoa ombi kwa wahisani wa kimataifa la kufadhiliwa msaada wa dharura wa dola milioni 34, ili kukidhi, halan, mahitaji ya umma wa Tarafa ya Ghaza, mahitaji ambayo yanaendelea kukithiri tangu mashambulizi kuanzishwa na vikosi vya Israel kwenye eneo mnamo tarehe 27 Disemba 2008.~~