Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

WFP yasihi mapigano yasitishwe ili itathminie mahitaji ya umma wa Ghaza

WFP yasihi mapigano yasitishwe ili itathminie mahitaji ya umma wa Ghaza

Hii leo, Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetoa mwito maalumu, kwa makundi yanayohasimiana katika eneo la Tarafa ya Ghaza, kusitisha mapigano na kuruhusu wahudumia misaada ya kiutu angalau kupata “upenu wa kupumua” utakaowawezesha kutathminia vyema mahitaji halisi ya umma waathirika katika Ghaza, ili baadaye kuwapatia wakazi hawo misaada ya kihali, ya kunusuru maisha.