12 Januari 2009
Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limeanzisha huduma ijulikanayo kama Operesheni za Kamba ya Kuokolea Ghaza, yenye lengo la kuhudumia watu wenye njaa ambao idadi yao inaendelea kuongezeka kila kukicha, tangu Israel kuanzisha mashambulio yake karibu wiki tatu zilizopita.