Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wajumbe wa kimataifa wakutana Roma kuandaa miradi ya kudhibiti bora maji duniani

Wajumbe wa kimataifa wakutana Roma kuandaa miradi ya kudhibiti bora maji duniani

Wajumbe wa kimataifa kutoka nchi 60 ziada wanakutana mjini Roma, Utaliana kwenye Makao Makuu ya Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) kuanzia leo tarehe 21 mpaka 23 Januari (2009) ambapo wataendelea kujadiliana mpango wa utendaji, unaohitajika kudhibiti bora matumizi ya maji ulimwenguni, kufuatia athari mbaya za mazingira zinazochochewa na mabadiliko ya hali ya hewa duniani.