Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mratibu wa UM juu ya Misaada ya Kiutu azuru Ghaza

Mratibu wa UM juu ya Misaada ya Kiutu azuru Ghaza

John Holmes, Mratibu wa UM juu ya Misaada ya Dharura na Masuala ya Kiutu ameanza ziara ya siku nne katika Israel na kwenye eneo liliokaliwa la WaFalastina la Tarafa ya Ghaza, kwa makusudio ya kutathminia mahitaji hakika ya kihali kwa waathirika wa operesheni za karibuni za majeshi ya Israel kwenye eneo hilo.