Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNFPA kuipongeza serikali mpya Marekani kwa kuchangisha tena misaada kwa Shirika

UNFPA kuipongeza serikali mpya Marekani kwa kuchangisha tena misaada kwa Shirika

Shirika la UM juu ya Udhibiti wa Idadi ya Watu UNFPA) limepongeza uamuzi wa Raisi Barack Obama wa Marekani kuanza tena kutoa mchango wa taifa lake, kufadhilia operesheni za UNFPA za kupunguza ufukara, kupunguza vifo vya watoto wachanga na kuimarisha uzazi bora kwa mama wazazi katika mataifa 154 ulimwenguni. ~ ~