27 Januari 2009
Benki muhimu maarufu inayohudumia Afrika ya Standard Bank, Ijumatatu imetiliana sahihi na Taasisi ya Mfuko wa Kimataifa Dhidi ya UKIMWI, kifua kikuu na malaria – inayoungwa mkono na UM – yaani Taasisi ya Global Fund, makubaliano ya kutoa huduma, bila malipo, za kusimamia matumizi ya misaada ya kupambana na majanga hayo matatu ya maradhi maututi wanayopokea mataifa husika katika Afrika.