Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Benki maarufu Afrika yaafikiana na UM kupiga vita pamoja maradhi maututi

Benki maarufu Afrika yaafikiana na UM kupiga vita pamoja maradhi maututi

Benki muhimu maarufu inayohudumia Afrika ya Standard Bank, Ijumatatu imetiliana sahihi na Taasisi ya Mfuko wa Kimataifa Dhidi ya UKIMWI, kifua kikuu na malaria – inayoungwa mkono na UM – yaani Taasisi ya Global Fund, makubaliano ya kutoa huduma, bila malipo, za kusimamia matumizi ya misaada ya kupambana na majanga hayo matatu ya maradhi maututi wanayopokea mataifa husika katika Afrika.