Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wapiganaji waasi wa Rwanda waliopo JKK wapatiwe fursa ya kurudi makwao, bila kulazimishwa, inasema UM

Wapiganaji waasi wa Rwanda waliopo JKK wapatiwe fursa ya kurudi makwao, bila kulazimishwa, inasema UM

Alan Doss, Mjumbe Maalumu wa KM kwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK) ameripotiwa akisema kwamba rai ya kuruhusu Wanyarwanda waliokuwa wakipigana na majeshi ya mgambo nchini Kongo kuzuru makwao na kuchunguza kama hali inafaa kwao kurejea, ni moja ya taratibu ambazo zikitekelezwa kama inavyopasa, zitasaidia kupunguza vurugu na uhasama unaofufuka mara kwa mara kwenye eneo la uhasama Kongo. Mradi huo, alisisitiza Doss, unabashiria “mapatano mema kati ya Serikali za Rwanda na JKK, yalioamua hatua za kuchukuliwa, zilizo salama,” za kuwarejesha makwao wale wapiganaji waliotokea Rwanda ikiwa wapiganaji hawo wataridhia kurejea kwa hiyari.