Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hapa na Pale

Hapa na Pale

Alan Doss, Mjumbe Maalumu wa KM kwa JKK, ameripoti kuridhia rasmi ombi la serikali ya Kongo la kutaka isaidiwe katika kuandaa mipango ya zile operesheni za pamoja za vikosi vya JKK/Rwanda dhidi ya waasi wa KiHutu kutoka Rwanda, waliopo kwenye eneo la mashariki. Uamuzi huu ulitolewa Ijumanne baada ya Doss kuzuru sehemu ya mashariki ya nchi, ambapo alipata fursa ya kutathminia athari za operesheni za vita kwa raia. Shuirika la Ulinzi Amani la UM katika JKK (MONUC) linatarajiwa kupeleka Goma, yalipo makao ya operesheni za vikosi vya JKK/Rwanda, timu ya maofisa wa kijeshi watakaowasiliana na kusaidia kupanga udhibiti bora wa operesheni zao, kwa makusudio ya kuwajumlisha watumishi wa kiraia watakaosimamia kadhia za kiutu kwa umma muhitaji kwenye eneo la uhasama.