MONUC itasaidia majeshi ya Rwanda/JKK dhidi ya waasi wa FDLR
Shirika la Ulinzi Amani la UM katika JKK (MONUC) limetoa taarifa yenye kueleza kwamba litatuma msaada wa usafiri na huduma za tiba kwa vikosi vya Rwanda na JKK ambavyo vinashirikiana kupambana na waasi wa KiHutu katika eneo la mashariki ya nchi, na ilisisitiza kwamba vikosi vya MONUC havitoshiriki kabisa kwenye operesheni hizo.