Skip to main content

UNRWA inakana tetesi zinazodai misaada kwa Ghaza hunyakuliwa na makundi haramu

UNRWA inakana tetesi zinazodai misaada kwa Ghaza hunyakuliwa na makundi haramu

Christopher Gunness, Msemaji wa Shirika la UM Linalofarajia Misaada ya Kiutu kwa WaFalastina wa Mashariki ya Karibu (UNRWA) ametoa taarifa maalumu yenye kukana zile tetesi zilizoenezwa kwenye vyombo vya habari, zenye kudai ya kwamba misaada ya UM, inayopelekwa kwenye eneo liliokaliwa la WaFalastina la Tarafa ya Ghaza huibiwa au hutekwa nyara [na makundi fulani ya kisiasa].