Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Idadi ya wasiokuwa na kazi ulimwenguni inaashiriwa kukithiri katika 2009, yahadharisha ILO

Idadi ya wasiokuwa na kazi ulimwenguni inaashiriwa kukithiri katika 2009, yahadharisha ILO

Shirika la UM juu ya Haki za Wafanyakazi (ILO) leo mjini Geneva limewasilisha ripoti ya mwaka yenye kuashiria muongezeko mkubwa wa idadi ya watu wasiokuwa na kazi katika 2009, kwa sababu ya kuselelea, kwa nguvu, kwa mizozo ya kiuchumi ulimwenguni.