Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Waasi wa LRA walihusika na mauaji ya raia katika JKK, OCHA imethibitisha

Waasi wa LRA walihusika na mauaji ya raia katika JKK, OCHA imethibitisha

Vile vile kuhusu JKK, Elizabeth Byrs, Msemaji wa Ofisi ya UM juu ya Misaada ya Dharura (OCHA) ametoa taarifa yenye kuthibitisha ya kuwa baina ya tarehe 1 hadi 20, Januari mwaka huu, waasi wa Uganda wa kundi la LRA waliosakama katika JKK, walishambulia mitaa 19 katika wilaya ya Haut Uele, kwenye jimbo la Orientale na kuua raia 269, na baadaye kufanya uharibifu wa mali, na kuiba pamoja na kuchoma moto nyumba za raia.