Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM unaihishimu Disemba mosi kuwa Siku ya UKIMWI Duniani

UM unaihishimu Disemba mosi kuwa Siku ya UKIMWI Duniani

Tarehe ya leo, Disemba mosi, inahishimiwa na jumuiya ya kimataifa kuwa ni Siku ya UKIMWI Duniani; na taadhima za mwaka huu zinakamilisha miaka 20 tangu UM kuanzisha kampeni ya kuhimiza Mataifa Wanachama kuchangisha huduma zao kupambana kipamoja na janga hili kote ulimwenguni. Kwenye ripoti iliotolewa na Jumuiya ya Muungano wa Miradi ya Mashirikia ya UM Dhidi ya UKIMWI (UNAIDS) ilikumbusha kwamba katika kipindi kilichomalizikia 2007, watu milioni 33 walikadiriwa kuwa wanaishi na virusi vya UKIMWI katika dunia.