Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wajumbe wa kimataifa waanza mazungumzo rasmi Poznan, Poland kuandaa mkataba mpya wa kuhifadhi mazingira

Wajumbe wa kimataifa waanza mazungumzo rasmi Poznan, Poland kuandaa mkataba mpya wa kuhifadhi mazingira

Katika mji wa Poznan, Poland leo kumeanza majadiliano ya wiki mbili, yanaongozwa na UM, kwenye Mkutano wa Mataifa Yalioridhia Mkataba wa Kudhibiti Bora Mabadiliko ya Hali ya Hewa Duniani, ambao makusudio yake hasa ni kuandaa maafikiano ya kusailiwa kwenye Mkutano Mkuu ujao, utakaofanyika 2009 kwenye mji wa Copenhagen, Denmark.