Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mratibu wa UM juu ya huduma za kiutu ahimiza misaada ziada kunusuru Wasomali na "ufukara uliotota"

Mratibu wa UM juu ya huduma za kiutu ahimiza misaada ziada kunusuru Wasomali na "ufukara uliotota"

Mratibu wa UM juu ya Misaada ya Kiutu kwa Usomali, Mark Bowden, kwenye mahojiano na waandishi habari wa kimataifa, yaliofanyika Makao Makuu, Ijumatano alasiri, alihadharisha kwamba bila ya wahisani wa kimataifa kuchangisha misaada ya dharura inayotakiwa kuuvua umma wa Usomali na mgogoro unaohatarisha maisha yao, kunaashiriwa idadi kubwa ya raia watakabiliwa na “ufukara kamili, wa kutota.”