Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Walimwengu wanaadhimisha Siku ya Kimataifa Kupiga Vita Ulaji Rushwa.

Walimwengu wanaadhimisha Siku ya Kimataifa Kupiga Vita Ulaji Rushwa.

Tarehe ya leo, Disemba 09, inaadhimishwa ulimwenguni kuwa ni Siku ya Kimataifa Kupiga Vita Ulaji Rushwa. Ofisi ya UM juu ya Udhibiti wa Uhalifu na Madawa ya Kulevya (UNODC) imeanzisha, kwenye siku hii, kampeni ya kuhimiza umma wa ulimwengu, katika sehemu zote za dunia, kuwa na msimamo imara dhidi ya matatizo ya ulaji rushwa kwenye maeneo yao.