Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kilimo cha umwagiliaji maji ndio ufunguo wa kudhaminia akiba ya chakula Afrika

Kilimo cha umwagiliaji maji ndio ufunguo wa kudhaminia akiba ya chakula Afrika

Kilimo cha umwagiliaji maji na usimamizi bora wa matumizi ya maji ndio “mambo muhimu” yatakayosaidia kukuza na kuimarisha akiba ya chakula katika mataifa ya Afrika, alisisitiza Jacques Diouf, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika kla UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) kwenye hotuba yake ya ufunguzi, alioitoa leo hii kwenye mkutano wa siku tatu ulioanza Sirte, Libya, kuzingatia Udhibiti wa Maji kwa Kilimo na Nishati katika Afrika.