Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

EU yaanzisha ulinzi wa muda mrefu wa misaada ya kunusuru maisha Usomali

EU yaanzisha ulinzi wa muda mrefu wa misaada ya kunusuru maisha Usomali

Shirika la UM juu ya Miradi ya Chakula Duniani (WFP) limetoa taarifa ya kuushukuru Umoja wa Ulaya (EU) kwa kupeleka manowari kwenye mwambao wa Usomali zitakazolinda zile meli zilizobebeba shehena ya misaada ya chakula dhidi ya maharamia.