Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mastakimu ya muda yanaandaliwa Sudan Kusini na UNHCR kwa wahamiaji wa JKK

Mastakimu ya muda yanaandaliwa Sudan Kusini na UNHCR kwa wahamiaji wa JKK

Katika taarifa nyengine, UNHCR inajiandaa kupokea wahamiaji wanaolekea Sudan Kusini hivi sasa, kufuatia ripoti za kuanzishwa operesheni za pamoja za kijeshi zilizojumuisha vikosi vya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Uganda na kutoka Sudan Kusini, askari ambao wana lengo la kuwafyeka kutoka mafichoni waasi wa Uganda wa kundi la LRA, waliojizatiti kwenye maeneo yaliopo kaskazini-mashariki ndani ya JKK, kwenye Mbuga ya Taifa ya Garamba.