Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

'Utambuzi wa mfumo wa ujinsiya utegemee sera za kitaifa na usishurutishwe kimataifa', nchi wanachama zakumbushana

'Utambuzi wa mfumo wa ujinsiya utegemee sera za kitaifa na usishurutishwe kimataifa', nchi wanachama zakumbushana

Kwenye majadiliano yaliofanyika Alkhamisi katika ukumbi wa Halmashauri ya Baraza Kuu juu ya Uchumi na Jamii (ECOSOC) kuzingatia “haki za binadamu, utambulishi wa kijinsiya na ujinsiya”, kulipigwa kura, isiyokuwa na masharti ya kiseheria, ambapo Mataifa Wanachama 66 yalitoa mwito wa kutaka kufutwa kwenye sheria zile amri zinazotafsiri vitendo vya ubasha, usagaji na usenge kuwa ni uhalifu. Kikao hiki kilidhaminiwa na balozi za mataifa ya Argentina, Brazil, Croatia, Gabon na pia Norway, Ufaransa na Uholanzi