Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ofisa wa WHO anasema hali ya afya Zimbabwe inashtusha

Ofisa wa WHO anasema hali ya afya Zimbabwe inashtusha

UM umeripoti idadi ya vifo Zimbabwe sasa hivi kutokana na maradhi ya kipindupindu imezidi 1,100. Dktr Dominique Legros, Ofisa wa Shirika la Afya Duniani (WHO), ambaye alikuwa Zimbabwe karibuni aliwaambia waandishi habari Geneva Ijumaa kwamba huduma za afya zimeharibika sana nchini na mahospitali yanafanana na mahame ya vizuka na pepo, kwa sababu wahudumia afya hawalipwi na wameamua kutokwenda kazini. Dktr Legros anatupatia maelezo zaidi: